Askofu Wanjiru kusalia korokoroni kwa siku 5, zaidi

Na Beatrice Maganga

Mwaniaji ugavana kwenye Kaunti ya Nairobi, Askofu Margaret Wanjiru ataendelea kusalia korokoroni kwa siku tano zijazo baada ya mahakama kupinga ombi lake la kuachiliwa kwa dhamana. Wanjiru alifikishwa mahakamani mapema leo akikabiliwa na tuhuma za kuzua vurugu na kuharibu mali, mashtaka ambayo ameyakana.
Wanjiru ni mmoja wa wanaowania ugavana kwa tiketi ya Jubilee, Kaunti ya Nairobi.
Alikamatwa jana baada ya yeye na wafuasi wake kukivamia kituo cha kura cha City Park na kuharibu karatasi za kupiga kura.