×
App Icon
The Standard e-Paper
Smart Minds Choose Us
★★★★ - on Play Store
Read on the App

Jubilee yaahirisha uteuzi katika kaunti 11

Na Carren Omae
Kinyume na ahadi ya viongozi wake, uteuzi wa Chama cha Jubilee ambao umeanza Ijumaa kwenye kaunti 21 nchini umekumbwa na sarakasi za kila aina. Ilianzia kucheleweshwa kwa vifaa vya uchaguzi, malalamishi ya wapigakura na wawaniaji sawia, vurugu, madai ya udanganyifu na kuharibiwa kwa vifaa vya kura, bila kusahau taarifa ya kujaribu kuficha uhalisia kutoka kwa chama hicho. Aidha uteuzi huo ulicheleweshwa hadi adhuhuri kwenye maeneo takribani yote.
Sasa hatima ya yote imekuwa kusitishwa kwa uteuzi kwenye kaunti 11, ikizingatiwa kuwa kwenye kaunti 25 zilizosalia, shughuli hiyo itafanyika Jumanne wiki ijayo, na Nairobi siku ya Jumatatu.
Kivumbi kilitifuka wakati wa uteuzi wa Jubilee leo hii. Ni hali iliyosababisha kuahirishwa kwa shughuli hiyo katika kaunti 11 ambazo ni: Narok, Kajiado, Kericho, Bomet, Uasin Gishu, Trans Nzoia, Baringo, Nakuru, Elgeyo Marakwet, Embu na Nandi.  Kaunti nyingine ni Kiambu, Laikipia, Meru na Pokot Magharibi.

Katibu Mkuu wa Jubilee, Raphael Tuju hata hivyo licha ya sarakasi na malalamishi kutolewa, uteuzi utaendelea kwenye kaunti za Murang’a, Kirinyaga, Nyeri na Nyandarua. Kaunti nyingine ambazo uteuzi umeendelea ni Meru, Uasin, Tharaka Nithi, Kiambu na Taita Taveta jumla zikiwa kaunti 10.

Get Full Access for Ksh299/Week
Bold Reporting Takes Time, Courage and Investment. Stand With Us.
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in