×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]
Premium

Charles III Atawazwa rasmi kuwa Mfalme wa Uingereza

News

Hatimaye Charles II mwenye umri wa miaka 74, ametawazwa kuwa Mfalme wa Uingereza. Shughuli ya kumtawaza mfalme huyo wa Uingereza imefanyika huku utawala wa kifalme nchini humo ukikabiliwa na upinzani.

Mfalme Charles wa tatu akichukua utawala kutoka kwa mamake Malkia Elizabeth wa, aliyefariki dunia Septemba mwaka jana baada ya kutawala kwa takriban miaka sabini.

Kabla ya kutawazwa Mfalme Charles wa tatu amekula kiapo kisha akaomba kwa sauti hivyo kumfanya kuwa wa kwanza kufanya hivyo miongoni mwa watawala arobaini tangu mwaka wa elu moja sitini na sita. 1066.

Askofu mkuu wa Canterbury Justin Welby ameongoza hafla hiyo ambayo imefanyika katika kanisa la Westminster Abbey

Mamilioni ya watu nchini Uingereza na kwingineko duniani wamefuatilia hafla hiyo ya kipekee inayojumuisha mipangilio ya kidini na tamaduni na ambayo inafanyika kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka sabini na minne.

Rais William Ruto ni miongoni mwa viongozi wa Afrika ambao wako Uingereza kwa hafla hiyo. Marais wengine ni Paul kagame wa Rwanda, Lazarus Chakwera wa Malawi na George Weah wa Liberia. Waziri Mkuu wa Cameroon Joseph Dion Ngute amemwakilisha Rais Paul Biya kwenye hafla hiyo.

Aidha Rais Emmerson Mnangagwa amekuwa kiongozi wa kwanza wa Zimbabwe kuzuru London kwa zaidi ya miongo miwili baada ya Uingereza kuiwekea vikwazo nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika.

Mwanzoni mwa hafla hiyo Graham Smith, kiongozi wa kundi linalopinga ufalme jijini London alikuwa miongoni mwa watu sita ambao walikamatwa.

Smith anayeliongoza vuguvugu la kisiasa la Republican wanaopinga utawala wa Kifalme, anadai unawawakilisha watu wenye uwezo na ukosefu wa usawa katika taifa linaloendelea kuota mizizi ya umasikini na mgawanyiko wa mahusiano ya kijamii.

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week