Mkurugenzi Mkuu Chama cha Azimio la Umoja One Kenya Raphael Tuju amevunja kimya chake kuhusu madai yaliyoibuliwa katika hati kiapo ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi IEBC Wafula Chebukati kwenye rufaa ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais.
Katika kikao na wanabari, Tuju ambaye amekiri kukutana na Chebukati amejitetea akisema walikutana naye akiwa na watu wengine na hivyo madai ya kuwa alilenga kushawishi matokeo ya uchaguzi ni uongo.