Mbunge wa Mathira, Ragathi Gachagua ameitaka Idara ya Upelelezi, DCI kukoma kuingiza siasa katika uchunguzi wa kifo cha mwanawe Mbunge Maalumu, David Ole Sankok.
Badala yake, Gachagua ameitaka DCI kuruhusu familia ya Sonkok kuomboleza kifgo cha Mumesi Sanko ambaye anadaiwa kujiua kwa kujipiga risasi wiki iliyopita nyumbani kwao.
Akizungumza leo alipoifariji familia ya Sankok, Gachagua amesema licha ya kuwa uchunguzi haujakamilika \DCI inastahili kuendeleza uchunguzi wa kimya na kukoma kuendelea kuishinikiza familia kurekopdi taarifa zaidi.
Sankok alihojiwa kwa mara ya pili siku ya Alhamisi kuhusu kifo cha mwanawe sawa na baadhi ya watu wa familia yake.
Polisi wanaendelea kuchunguza bunduki mbili za Sankok shotgun na Ceska kubaini ni ipi marehemu mwenye umri wa miaka kumi na mitano anadaiwa kuitumia kujiua.