Raia sita zaidi wa kigen wamekamatwa katika Kaunti ya Garissa wakiarifiwa kuwa na lengo la kusafiri kuelekea Somalia.
Kwa mujibu wa polisi, raia hao wa kigeni walikamatwa wakiwa katika harakati za kuulizia njia mwafaka ya kufika Somalia kupitia mpaka ulioko katika kaunti hiyo.
Baada ya kuhojiwa 6 hao wamekiri kwamba walikuwa wanalenga kujiunga na kundi la kigaidi la Alshabab baada ya kusajiliwa kutoka Tanzania na Uganda.
Takriban wiki mbili zilizopita, raia watatu wa kigeni kutoka Tanzania walikamatwa katika Kaunti ya Garissa baada ya wakazi kudokezea polisi.
Watatu hao walitambuliwa kama Abdul Saif Salimu, Zuberi Ngare Mtondoo na Seif Abdalla Juma.