Mbunge wa Kabuchai Majimbo Kalasinga na mwenzake wa Webuye Mashariki Dan Wanyama wamewaongoza wakazi wa Chwele katika Kaunti ya Bungoma kufanya maandamano ya amani kulalamikia ongezeko la visa vya ajali kwenye maeneo bunge hayo.
Waandamanaji walifunga Barabara Kuu ya Lwakhakha - Chwele - Bokoli na kuzuia matrela yanayopita kwenye barabara hiyo wakisema ni chanzo cha visa vya ajali hizo.
Viongozi hao wanasema barabara hiyo ilitumika wakati wa janga la covid 19 ili kupunguza msongamano kwenye mpaka wa Malaba ila imeendelea kutumika baada ya msongamano huo kuisha.