×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]

Hakuna Mgawanyiko Kenya Kwanza-Asema Gachagua

News

Naibu wa Rais Rigathi Gachagua ameendelea kuwashauri wanasiasa wa eneo la Kati ya Nchi kuunga mkono serikali iliyopo kwa manufaa ya wakazi wa Mlima Kenya.

Akizungumza katika kaunti ya Nyeri alipoongoza halfa ya kufuzu kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mt. Kenya, Naibu huyo wa Rais, amesisitiza kwamba sasa msimu wa siasa umeisha na kwamba kuna haja ya viongozi wa matabaka mbalimbali kuungana.

Wakati uo huo, Gachagua amepuuza madai kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwa viongozi wa muungano wa Kenya Kwanza.

Gachagua amesema tofauti zilizoshuhudiwa wakati wa uchaguzi wa wawakilishi wa Kenya Kwanza katika Bunge la Afrika Mashariki EALA, hauwezi kusababisha mgawanyiko wowote.

Kauli ya Gachagua inajiri kufuatia taarifa kwamba baadhi ya viongozi wa eneo la Mlima Kenya hawakufurahishwa na majina ya waliopendekezwa kuwa wabunge wa EALA katika mrengo huo wa Kenya Kwanza kwa kuwa hawakuwajumuisha wawakilishi kutoka eneo la Mlima Kenya.

Wawakilishi wa Kenya Kwanza katika EALA ni aliyekuwa mwaniaji wa Ugavana katika kaunti ya Mombasa kwa tiketi ya UDA Omar Hassan Omar, aliyekuwa Mbunge Maalum David Ole Sankok, , Ziporrah Kering; Falhadha Dekow na Fred Muteti.

Related Topics


.

Popular this week

.

Latest Articles