Maafisa wa polisi wa kituo cha Longisa, katika Kaunti ya Bomet wanaendelea kumzuilia mvulana wa miaka kumi na mmoja anayedaiwa kukiri kumuua binamuye wa miaka saba.
Inadaiwa mvulana huyo amewaeleza polisi kuwa mamaye alimpenda binamu yake zaidi kulinganishwa na yeye.
Kamanda wa Polisi wa Bomet Esther Seroney amesema tayari uchunguzi umeanzishwa kabla ya hatua kuchukuliwa.