Tukio la Mswidi mpiga mbizi aliyejitolea kusaidia katika juhudi za kuopoa miili ya mama na mwanawe waliozama baharini kutangaza kushindwa kwake kufaulu kama alivyo kuwa ameahidi mwanzoni limezua gumzo kubwa miongoni ya Wakenya.
Gumzo hilo limejaa shaka na dhana kwamba huenda mzungu huyo hakushindwa kupata gari yenyewe humo baharini ila huenda alinyoroshwa na mkono wa chuma wa serikali kueleza Wakenya kwamba hakufaulu.