Nyundo ya waziri wa usalama Fred Matiang’i ilipo gonga kufuatia agizo lake kutangaza vita dhidi ya madawa ya kulevya, operesheni ya polisi mara moja ikaanza.
Aidha kamata kamata pamoja na misako ya makaazi ya washukiwa ikatanda mjini Mombasa ambapo zaidi ya watu 15 wakaarifiwa kutiwa mikononi kwa shutuma za kuendeleza biashara ya mihadarati.