Naibu wa Rais William Ruto.
Hamkani si shwari tena. Wasemavyo Waswahili, akufukuzaye hakwambii toka. Tamko la Rais Uhuru Kenyatta hivi majuzi kwamba hajali ni nani atakayemrithi mwaka wa 2022 ni ishara tosha kwamba ufa kati yake na naibu wake William Ruto unazidi kupanuka na huenda stakabadhi ya kifo cha Jubilee ikatiwa saini kabla ya uchaguzi mkuu ujao.