Mdahalo umezuka tangu kuteketezwa kwa mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Safaricom, Robert “Bob” Collimore na wakenya wengine mashuhuri hivi karibuni kuwa sababu yake halisi ya kupitia mfumo huo ni nini haswa. Wakenya hao mashuhuri ambao miili yao ilipitia mfumo huo ni pamoja na aliyekuwa mwanaharakati wa uhifadhi wa Mazingira Bi. Wangari Maathai aliyefariki mwaka 2011, aliyekuwa kiongozi wa upinzani Keneth Matiba, aliiyekuwa mchezaji golf maarufu Peter Njiru, aliyekuwa waziri Peter Okondo, Askofu wa Kanisa la Kianglikana Manasses Kuria na mkewe Nyambura Kuria.
Mwaka uliopita John Macharia mwana wa mkurugenzi wa Royal Media S.K Macharia aliyefariki mwaka uliopita baada ya kuhusika katika ajali ya barabarani mwili wake pia ulitekeketwa badala ya mazishi ya kawaida. Jambo la kustaajabisha ni kwamba katika shughuli za watu hao wote sherehe za kuteketeza miili zimehudhuriwa tu na familia na watu wa karibu. Historia ya uteketezaji maiti Kuteketeza maiti kama sehemu ya mfumo wa mazishi kumefanyika tangu jadi zaidi ya miaka 10,000 iliyopita.