Wakati wabunge wa Mombasa walipokuwa wakijipiga kifua muda mfupi baada ya mkondo wa kwanza wa marekebisho ya sheria inayoruhusu biashara za meli na uchukuzi ya Merchant Shipping Act 2019 kupingwa na wabunge, hawakujua kwamba nguzo ya nchi ni Rais ambaye anapaswa kuingilia mahali ambapo walafi wameenda kombo kisheria.
Hata kabla ya kuidhinishwa rasmi na rais kuwa sheria, wabunge wa pwani wakiongozwa na kijana wao wa mkono katibu mkuu wa chama cha makuli nchini cha Dock Workers Union, Simon Sang, tayari walikuwa wanatafuta ukumbi wa kuandaa sherehe za kufaulu kufi lisi ndoto ya vijana 1000 ambao walikuwa wanasubiri kuajiriwa zaidi na kampuni ya meli ya MSC. Sang ambaye amekuwa dalali mkubwa katika kuwakutanisha baadhi ya wabunge na matajiri fulani wanaomezea mate kiegezo kinachong’ang’aniwa bandarini cha CT2, alikuwa mstari wa mbele kusaka sehemu ambayo ingewaleta viongozi wote kusherehekea ushindi wao.