×
App Icon
The Standard e-Paper
Join Thousands of Readers
★★★★ - on Play Store
Download Now

Eneo la Simba wala watu wa Tsavo

Wafanya kazi waliokuwa wakijenga reli katika enzi za ukoloni. [File, Pambazuko]

Mbuga ya kitaifa ya hifadhi ya Tsavo ndio kubwa zaidi nchini na ya pili kwa ukubwa duniani baada ya ile ya kitaifa ya Kruger iliyoka Afrika Kusini, ikiwa na ukubwa wa kilomita 21,000 mraba. Mbuga hii ambayo imegawanywa sehemu mbili ya Tsavo Mashariki na Magharibi ina sifa kemkem duniani kama hifadhi ya wanyama maarufu watano yaani Big Five ambao ni chui, ndovu, kifaru, simba na nyati. Hata hivyo simba wa mbuga ya Tsavo wanaotofauti na wale wengine ulimwenguni  kwani wale wa kiume hawana nywele nyingi kichwani , hivyo kuwa vigumu kidogo kuwatofautisha na wale wa kike.

 Fauku ya hayo simba wa Tsavo wana historia kabambe hasa wale simba wala watu wawili alimaarufu kama Man Eaters of Tsavo. Simba hawa ndio kiini cha jina la eneo liitawalo Man Eaters lililoko kwenye barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Nairobi, yapata  kilomita 40 kutoka mji wa Voi.

Get Full Access for Ksh299/Week
Uncover the stories others won’t tell. Subscribe now for exclusive access
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in