Aliyekuwa kinara wa Nasa Raila Odinga akimsalimu Naibu wa Rais William Ruto katika hafla iliyopita. [Picha: Standard]
Leo ukiambia andika nsha fupi isiyozidi maneno ishirini kuhusiana na sampuli za siasa za viongozi wawili wa Kenya, waitwao Raila Odinga na William Ruto, ukiwa mtaalam na mdadisi wa siasa ya Kenya, utaandika tu; Hali ya Raila, Hali ya Ruto! Mifano yao inajitokeza tangu miaka ya 1992/97 kwa Raila akiwa anashindana kisera za kisiasa na babake n ahata wazee wengine kwenye chama cha FORD. Ushindani wake Raila ulimsukuma kukataa kukaliwa chapatti chamani cha FORD Kenya na hatimaye kuanzisha chama chake cha NDP kabla ya kuungana na KANU na baadaye kuyeyukia mbali mkaribio wa uchaguzi mkuu wa 2002.