Kwa wale ambao ni wapenzi wa filamu za wasanii wa Nigeria bila shaka wamezowea kuona mila na utamaduni wa watu wa Nigeria zikiigizwa kwa mapana na marefu.
Kuna kiongozi wa ukoo Fulani ama mfalme ambaye huko kwao anajulikana kama Igwee na yeye ndiye anayefanya maamuzi yote na kutekeleza sheria kwa mujibu wa mila zao na huwa ndiye anayesikizwa na wote huku akiwa na serikali yake na baraza lake la mawaziri.