Huku watu wakibarikiwa na vipaji mbali mbali kama vile vya kuimba, kucheza, kuigiza na vinginevyo maarufu, Edward Alukuma mwenye umri wa miaka 38 ameajaliwa kuwa na kipaji cha kumeza ugali kisawasawa utadhania unausunda kwenye kibuyu ilhali ni tumbo lake.
Anakula zaidi ya kilo kumi na mbili (12) za ugali kila siku, sawa na kuramba mifuko sita ya unga wa ugali ama nusu bandali la unga yeye peke yake. Wengi wanashangaa iwapo wake ni utumbo wa kawaida wa mwanadamu ama ni mabomba sawa nay ale yapitishayo maji. Alukuma ambaye ni mwenyeji wa Buyokha kaunti ndogo ya