Mwanasiasa mcheshi Kalembe Ndile ni mtu wa kawaida. Sawia na nguo ya kaniki, kamwe huwezi kumbadilisha jinsi alivyo kimazungumzo, maisha yake, msimamo wake katika kila jambo analonuia ama msukumo wowote unaokadiria kumyumbisha.
Bado haijulikani iwapo wazo ama hatua ya serikali ya Uhuru Kenyatta kumkumbuka mwanasiasa Kalembe Ndile pamoja na wenzake wa Ukambani kuteuliwa wakurugenzi wa mashirika hivi majuzi ni kutokana na huruma, malipo ya hisani ama msukumo kwamba rafiki ya Kalembe Ndile anachomwa na jua kali la pwani akihudumia wateja kwenye mkahawa wa mvinyo.