Hapa Kenya tumebarikiwa na wasanii wenye vipaji mbalimbali ambao tunafaa tujivunie uwepo wao katika maisha yetu. Tunao wasanii wa ucheshi, wanamziki na wengineo wanaotambulika sio hapa nchini pekee, bali pia kwenye mataifa mbali mbali ulimwenguni.
Tunao wanamuziki wanaoimba aina za kipekee za nyimbo kama vile Kapuka na Genge ambao kwa kawaida huimba kwa lugha ya mtaani maarufu Sheng. Wasanii wanaoimba kwa lugha za jamii mbali mbali za humu nchini kama vile Kijaluo, Kikuyu, Kikamba na Kiluhya pia wapo.