Mwanamke atoroka hospitalini Bungoma akiwa na dalili za virusi vya korona

Huenda mwanamke mwenye umri wa miaka 31 akafunguliwa mashtaka kwa kutoroka hospitalini alikokuwa amelazwa akiwa na dalili za virusi vya korona.

Mwanamke huyo aliyetambuliwa kwa jina Brenda Naliaka alikuwa akizuiliwa katika Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Kimilili, Bungoma baada ya kulazwa huko huku madaktari wakifuatilia hali yake ya afya.

Inaarifiwa kwamba alisafiri kutoka Nairobi mnamo Aprili mosi akiwa na dalili za kuugua hali iliyomfanya kuelekea hospitalini baada ya kuwasili Bungoma.

Hata hivyo alitoroka alipowekwa karantini na baadaye kupatikana nyumbani kwake katika kijiji cha Temba Temba na kurudishwa tena karantini huku matokeo ya sampuli zake yakisubiriwa.

Related Topics

korona Bungoma