Mwanahabari Jacque Maribe na mpenziwe, Joseph Kuria lrungu maarufu Jowie, wamesomewa upya mashtaka ya mauaji ya mfanyabaishara, Monica Kimani ambapo wamekana mashtaka dhidi yao.
Wawili hao wamekana kuhusika mauaji hayo mnamo Septemba 19 mwaka uliopita katika nyumba za Lamuria Gardens Mtaani Kilimani, jijini Nairobi , wakati Monica aliporejea nchini kutoka Sudan Kusini alikokuwa akijihusisha na biashara ya familia.
Katika mashtaka hayo mapya, upande wa mashtaka ulibadili stakabadhi za mahakama na kulijumuisha jingine la utani la Jowie ambalo ni Harun.