Cyril Ramaphosa apishwa rasmi kuwa Rais wa Afrika Kusini

Hatimaye Cyril Ramaphosa ameapishwa rasmi kuwa Rais wa Afrika Kusini. Ramaphosa mwenye umri miaka 66 alichaguliwa kwa asilimia 57.5 za kura na kunyakuwa viti 230 miongoni mwa 400 bungeni.

Uchaguzi huo ndio wakwanza kwa chama tawala cha ANC, kupata kura chini ya asilimia 60 tangu taifa hilo kupata uhuru, vilevile ndio mara ya kwanza kushudiwa idadi ndogo ya wapiga kura.

Ramaphosa alichukuwa wadhifa wa Kaimu Rais baada ya Rais Jacob Zuma kujiuzulu kufuatia madai ya ufisadi. Ramaphosa ni miongoni mwa viongozi amabao waliousika pakubwa katika uwaniaji wa Uhuru katika taifa hilo.