Oparesheni kali ya Usalama inatarajiwa kuanza eneo la North Rift baada ya maafisa wa polisi kutumwa eneo hilo. Waziri wa Usalama na Masuala ya Ndani ya Nchi Fred Matiangi amewatuma maafisa hao wakiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Maafisa wa Kukabili Ghasia GSU kiongoza oparesheni kwenye kaunti za Baringo, Pokot Magharibi, Samburu, Elgeyo Marakwet, Turkana na Laikipia.
Haya yanajiri kufuatia uvamizi baina ya jamii kwenye kaunti hizo ambao umesababisha watu kadhaa kuuliwa na mali kuharibiwa. Kadhalika watu kadhaa wamehama makazi hayo. Hapo jana Gavana wa Pokot Magharibi John Lonyangapuo alikutana na mwenzake wa Elgeyo Marakwet, Alex Tolgos walikutana ili kujadili jinsi ya kurejesha manai huku Lonyangapuo akiwalaumu maafisa wa polisi kwa kukwepa maeneo yenye mizozo hasa msitu wa Embobut.