Saa chache tu baada ya Bweni la Shule ya Upili ya Wasichana ya Gekomoni kuteketea mapema leo Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Thomas Nyaencha amekiri kwamba wanafunzi wengi walikuwa wakilala katika bweni hilo kuzidi idadi inayostahili.
Akiwahutubia wanahabari shuleni humo Nyaencha aidha amelalamikia hatua ya serikali ya Kaunti hiyo kutokarabati barabara zinazopita nyuma ya shule hiyo hali iliyowapa ugumu maafisa wa kuzima moto wa kaunti kufika shuleni humo ili kuukabili moto huo ulioketeza mali ya thamani ya shilingi milioni 1.2.