Idadi ya wanafunzi waliokuwa katika bweni lililoteketea Nyamira yatajwa kuwa kubwa.

Saa chache tu baada ya Bweni la  Shule ya Upili ya Wasichana ya Gekomoni kuteketea mapema leo Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Thomas Nyaencha amekiri kwamba wanafunzi wengi walikuwa wakilala katika bweni hilo kuzidi idadi inayostahili.

Akiwahutubia wanahabari shuleni humo Nyaencha aidha amelalamikia hatua ya serikali ya Kaunti hiyo kutokarabati barabara zinazopita nyuma ya shule hiyo hali iliyowapa ugumu maafisa wa kuzima moto wa kaunti kufika  shuleni humo ili kuukabili moto huo ulioketeza mali  ya thamani ya shilingi milioni 1.2.