Mafuriko yatatiza usafiri kwenye barabara ya Kakuma-Lokichogio

Usafiri kwenye barabara ya Kakuma - Lokichogio, Kaunti ya Turkana umetatizika kufuatia mafuriko ya mvua kubwa iliyonyesha katika eneo hilo usiku wa kuamkia leo.

Maafisa wa Shirika la Msalaba Mwekundu wamesema barabara hiyo imefurika na hivyo kuwa vigumu kwa magari na hata binadamu kupita na kwamba huenda hali ikawa mbaya zaidi iwapo mvua itaendelea kunyesha.

Taarifa hii inajiri wiki kadhaa tu baada ya viongozi na mashirika mbalimbali kutoa msaada wa vyakula, dawa na maji kwa wakazi wa Kaunti ya Turkana walioathirika na baa la njaa kutokana na kiangazi.