Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Smart Minds Choose Us
★★★★ - on Play Store
Download App

Maafisa wa Kukabili Ugaidi, waruhusiwa kumzuilia kwa siku 15 dereva wa gari lililokuwa limewabeba madaktari wawili wa Cuba

Maafisa wa Kukabili Ugaidi, ATPU wameruhusiwa kumzuilia kwa siku 15 dereva wa gari lililokuwa limewabeba madaktari wawili wa Cuba waliotekwa nyara Ijumaa wiki iliyopita na watu wanaoshukiwa kuwa wa kundi gaidi la Alshabab.
 
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Milimani, Muthoni Nzibe,  ametoa agizo hilo baada ya upande wa mashtaka kuomba kwamba mshukiwa Isaack Ibrein Robow anapaswa kuzuiliwa zaidi kuruhusu uchunguzi.
 
Mshukiwa alikamatwa tarehe 12 mwezi huu Mjini Mandera kisha kusafirishwa hadi jijini Nairobi Jumapili wiki hii ili kufikishwa mahakamani.
 
Idara ya uchunguzi inalenga kujua iwapo mshukiwa alishirikiana na magaidi kufanikisha utekaji nyara wa madaktari hao. Iwapo atapatikana na hatia, atahukumiwa kifungo cha miaka 20 jela.
 
Haya yanajiri huku madaktari wanne wa Cuba waliokuwa wakihudumu katika Kaunti za Lamu na Tana River  wakiondoka eneo hilo kwa kuhofia usalama wao. 

Wikendi, madaktari wawili wanne waliokuwa wakihudumu katika Kaunti  za Garrisa na Wajir walisafirishwa hadi hapa Nairobi baada ya wenzao wawili waliokuwa wakihudumu katika Kaunti ya Manderea kutekwa nyara.

Maafisa wa usalama  kwa sasa wanaendelea juhudi za kuwakomboa wawili hao Landy Rodriguez na Assel Herera Correa ambao walivushwa nchini Somalia baada ya kutekwa nyara Ijumaa wiki iliyopita.

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News

Related Topics