Maafisa wa polisi Jijini Mombasa, wanaendelea kuwazuilia washukiwa tano wanaohusisha na mauji ya mtu mmoja na misururu ya visa vya wizi katika eneo la Makande Kaunti ya Mombasa.
Washikiwa hao walinaswa kwenye Kamera za CCTV ambayo ilitumwa kwa ofisi ya DCI, wakioneka wakimwibia mwanamke mmoja wakiwa na bunduki. Aidha watatu miongoni mwao, walionekana wakitoroka katika eneo la tukio kwa pikipiki ambayo imenaswa na polisi.
Kamanda wa Polisi kaunti ya Mombasa Johnston Ipara, amesema kwamba washukiwa hao walikamatwa maeneo ya
Aidha amesema Polisi wanaendelea kuwatafuta washukiwa wengine, ambao wanaishi maeneo ya Mikindani, Chaani na Migadini.
Watano hao wanazuiliwa kwenye kituo cha Polisi cha Changamwe, wakisubiri kufikishwa mahakamani kesho kufunguliwa mashtaka.
...