Washukiwa 5 waliohusishwa na mauaji wazuiliwa mjini Mombasa

Maafisa wa polisi Jijini Mombasa, wanaendelea kuwazuilia washukiwa  tano wanaohusisha na mauji ya mtu mmoja na misururu ya visa vya wizi katika eneo la Makande Kaunti ya  Mombasa.

Washikiwa hao walinaswa kwenye Kamera za  CCTV ambayo ilitumwa kwa ofisi ya DCI, wakioneka wakimwibia mwanamke mmoja wakiwa na bunduki.  Aidha watatu miongoni mwao, walionekana wakitoroka katika eneo la tukio  kwa  pikipiki ambayo imenaswa na polisi.

Kamanda wa Polisi kaunti ya Mombasa Johnston Ipara, amesema kwamba washukiwa hao  walikamatwa maeneo ya  Mtwapa, Chaani  na Kibarani usiku wa kuamkia leo.

Aidha amesema Polisi wanaendelea kuwatafuta washukiwa wengine, ambao wanaishi maeneo ya Mikindani, Chaani na Migadini.

Watano hao wanazuiliwa kwenye kituo cha Polisi cha Changamwe,  wakisubiri kufikishwa mahakamani kesho kufunguliwa mashtaka.

...

Related Topics