Wafanyabiashara kwenye Kaunti ya Mombasa wameeleza kukerwa na hatua ya Usimamizi wa Mamlaka ya Kitaifa ya Mazingira, NEMA kutangaza kwamba itapiga marufuku mifuko inayotumika kubebea mizigo, marufuku ambayo yataanza kutekelezwa mwishoni mwa mwezi Machi
Kulingana nao, NEMA haijakuwa ikiwahusisha watengenezaji wa mifuko hiyo ili kuafikiana kuhusu suala la ni vipi mifuko ya kudumu itatengenezwa kwani ya sasa inaarifiwa kuwa isiyoafikia viwango.