Wakili anayedaiwa kumpiga risasi mwanawe akimbizwa Hospitalini baada ya kuugua ghafla

Wakili  Assa Nyakundi anayedaiwa kumpiga risasi bila kukusudia hadi kufa mwanawe mwenye umri wa miaka 29 amekimbizwa katika Hospitali ya Nairobi baada ya kuugua ghafla kufuatia shinikizo la damu.

Maafisa hao wa Kitengo cha Upelelezi, DCI wanachunguza jinsi wakili huyo anadai kumpiga risasi mwanawe wakiwa nyumbani kwao katika mtaa wa Muthaiga. Alipomatawa, Nyakundi ambaye ana leseni ya kumiliki silaha alidai kuwa alifyetua risasi iliyompiga mwanawe kifuani bila kukusudia muda mfupi baada ya wao kurejea nyumbani kutoka kanisani.

Kisa hicho kiliripotiwa katika Kituo cha Polisi cha Muthaiga huku ikiarifiwa kuwa wakili huyo alikuwa akirejesha bastola yake kwenye kipochi ndani ya gari kabla ya kufyetua risasi hiyo na kumuua mwanawe Joseph Nyakundi aliyekuwa amekalia kiti cha nyuma cha gari hilo.

Tayari bastola hiyo pamoja na risasi 14 imechukuliwa.

Related Topics