Wakazi wa Kaunti ya Nyamira wametakiwa kukomesha kutumia umeme kwa njia haramu

Wakazi wa Kaunti ya  Nyamira wametakiwa kukomesha tabia ya kutumia umeme kwa njia haramu. Meneja wa Kampuni ya usambazaji umeme nchini, Kenya Power tawi la Nyamira, Dan Machuka amesema hali hiyo inachangia pakubwa katika kufeli kwa mitambo ya transfoma mara kwa mara, hali ambayo inaathiri shughuli za maendeleo kwenye eneo hilo.

Machuka amesema wameanzisha msako mkali wa kuwanasa wahusika kisha kuwafungulia mashtaka mahakamani.

Kauli ya Machuka inajiri baada ya kituo hiki kubaini kuwa baadhi ya wakazi wa  kaunti hiyo wamejiunganishia nguvu za umeme kwenye  makazi bila kuzingatia taratibu mwafaka hali inayo hatarisha maisha yao.

Related Topics