Kwa mara nyingine Seneta wa Baringo, Gideo Moi amezungumzia siasa za mwaka 2022 akisema kuwa wakati huu ni wa kuwahudumia wananchi wala si kujihusisha na siasa za uchaguzi ambao bado haujawadia. Moi aliyasema hayo katika mahojiano na Runinga na KTN.
Akizungumzia mabadiliko ya Katiba, Moi amesema Wakenya wana haki kisheria kufanya mabadiliko kwani yatachangia vita dhidi ya ufisadi.