Raila ateuliwa na AU kuongoza ujenzi wa muundo-msingi, Afrika

Umoja wa Afrika leo umetengaza uteuzi wa Kiongozi wa Chama cha ODM Riala Odinga katika wadhfa wa msimamizi wa ujenzi wa Muundo Msingi barani Afrika. Katika taraifa mwenyekiti wa umoja huo  Moussa Faki amesema Raila atashirikiana na umoja huo kuimarisha juhudi zake katika muundo msingi.

Raila katika wadhfa huo pia amejukumiwa kutafuta uungwaji mkono kutoka kwa viongozi wa kisiasa na kiuchumi kufanikisha moango huo.

Rais Uhuru Kenyatta amempongeza Raila kwa uteuzi huo. Rais amesema uteuzi huo usingeweza kufanikiwa iwapo wasingekubali kuweka kando tofauti zao za kisiasa na kushirikiana kufanya kazi pamoja kwa manufaa ya wananchi.

Aidha ameongeza kuwa uteuzi huo utakuwa na manufaa makubwa kwa taifa kwani wakati Raila atakapokuwa akiongoza kitengo hicho hatasahau changamoto zinazokumba Kenya katika masuala ya muundo msingi.

Kwa upande wale Raila amesema amekubali uteuzi huo, kufuatia ombi kutoka kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Mousa .