Rais Uhuru Kenyatta amefanya uteuzi mpya serikalini ambapo amemteua aliyekuwa Spika wa Seneti, Ekwe Ethuro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, HELB wadhifa atakaoushikilia kwa kipindi cha miaka 5. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, IEBC Isaack Hassan ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Viwanda.
Mjane wa aliyekuwa Afisa Mkuu Mtendaji wa Tume ya Uchaguzi, IEBC Chris Musando, Eva Buyu Musando aidha ameteuliwa kuwa mwanachama wa Mamlaka ya kushughulikia usafirishaji wa bidhaa hadi mataifa ya nje. Ameteuliwa pamoja na Kisoi Munyao na John Masaba. Aliyekuwa Seneta wa Kitui, David Musila ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Makavazi ya Kitaifa.