Gavana wa Nairobi Mike Sonko amewashtumu wale wanaoikosoa hatua yake ya kuwafuta wafanyakazi wa kaunti ambao ni fisadi. Sonko amesema ataendelea na uchunguzi na iwapo kuna wafanyakazi watakaohusishwa na visa vyovyote wa ufisadi wataachishwa kazi. Amesema jumla ya wafanyakazi sitini wametambulika na kwamba watachukuliwa hatua za kisheria.
Wakati uo huo, amewaonya wawakilishi wadi anaodai wamelipwa ku mhangaisha ili aitimize lengo hilo.