Na Beatrice Maganga
Kwa siku ya pili leo hii, Rais Uhuru Kenyatta amezishtumu idara za serikali zisizozingatia utekelezaji wa majukumu hasa katika kukabili ufisadi na badala yake kulaumiana. Akizungumza mapema leo wakati wa halfa ya kumwapisha Jaji Mkuu mpya David Maraga, Rais amesema ni japo la kusikitisha kwa idara mbalimbali kukwepa kuwajibikia masuala mbalimbali na kuzilaumu nyingine.