Kenya ya sasa isingekuwa Kenya bila juhudi za baadhi ya wananchi walioona umuhimu wa kupiga vita ukoloni mambo leo, ujakazi, ukosefu wa elimu na mengine mengi.
Hivyo ni aibu kubwa pale mtu aliyeteswa gerezani, mtu aliyepigania mabadiliko ya katiba na hata kuiweka ukabila pembeni na kusema “kibaki tosha’’ anapodhalilishwa na kuonekana kama asiyekuwa na umuhimu kwa taifa hili.