×
App Icon
The Standard e-Paper
Join Thousands Daily
★★★★ - on Play Store
Download App

Mvutano wachacha bungeni kuhusu VAT

Hatimaye Spika wa Bunge la Kitaifa, Justine Muturi ametangaza kuidhinishwa kwa mapendekezo ya Rais Uhuru Kenyatta ya kupunguza thamani ya kodi ya ziada kutoka asilimia 16 hadi asilimia 8 licha ya pingamizi kutoka kwa wabunge kuhusu namna shughuli ya kupiga kura ilivyoendeshwa. Kikao cha kujadili marekebisho hayo kilishamiri vurumai wakati wabunge walipoangizwa kupiga kura kwa mara nyingine licha ya awali kuangusha mapendekezo ya Rais. Aidha Kiongozi wa Wengi katika bunge hilo, Adan Duale na mwenzake wa Wachache, John Mbadi walizomewa na wabunge huku wakishtumiwa kwa madai ya kuwachochea wabunge wengine kuondoka katika majengo ya bunge ili wasifikishe idadi inayohitajika ya kuangusha mapendekezo ya Rais.

Ndivyo hali ilivyokuwa baada ya Mwakilishi wa Kike wa Kaunti ya Narok, Soipan Tuya kutangaza kwamba idadi ya wabunge waliokuwa katika majengo ya bunge ilikuwa 215, ilhali idadi inayohitajika ni wabunge 233, hivyo kupita kwa mswada wa marekebisho yaliyopendekezwa na Rais kwa mujibu wa sheria za bunge.  Awali kura ilipopigwa, upande wa wanaopinga uliibuka mshindi katika kura hiyo.

Get Full Access for Ksh299/Week.
Fact‑first reporting that puts you at the heart of the newsroom. Subscribe for full access.
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in

Related Topics

Uhuru Muturi