Please enable JavaScript to view advertisements.
×
App Icon
The Standard e-Paper
Kenya’s Boldest Voice
★★★★ - on Play Store
Download App

Laboso asema kipengee cha kuwazuia wanasiasa kuhama vyama kilikuwa kandamizi

Na, Beatrice Maganga

Baada ya kusitishwa jana, hatimaye Bunge la Kitaifa limerejelea mjadala kuhusu ripoti ya Kamati ya Pamoja iliyojadili hatma ya makamishna wa Tume ya Uchaguzi, IEBC na mfumo wa uchaguzi kwa ujumla, baada ya Naibu Spika Joyce Laboso kuidhinisha marekebisho kwenye kipengele ambacho kingewazuia wanasiasa kuvihama vyama vyao wanaposhindwa katika uteuzi wa kuwania nyadhifa mbalimbali.
Akitoa uamuzi huo kwenye kikao cha alasiri, Laboso amesema kipengee hicho kinakiuka haki za wawaniaji wa viti mbalimbali vya kisiasa.Hata hivyo amewashauri wabunge kutafuta ushauri wa viongozi wao iwapo wanahitaji mabadiliko zaidi ikizingatiwa kuwa ripoti hiyo iliandaliwa na wajumbe wa CORD na Jubilee.
Licha ya kuunga mkono ripoti hiyo baada ya kufanyiwa marekebisho, Kiongozi wa Wengi katika Bunge la Taifa, Adan Duale amesema hulka ya kuhama vyama ni mtindo usiyofaa. Kiongozi wa Wachache katika bunge hilo, Francis Nyenze kwa upande wake ameuunga mkono uamuzi huo wa spika akisema ni wa busara. Wabugne wengine aidha wamedai kwamba huenda watu waliokijumuisha kipengele cha kuzuia kuhama kutoka kwa chama kimoja hadi kingine walikuwa na njama fiche.
Awali Rais Uhuru Kenyatta na Kinara wa CORD Raila Odinga waliipitisha ripoti hiyo iliyoandaliwa na Kamati iliyoongozwa na maseneta, James Orengo na Kiraitu Murungi jinsi ilivyo. Seneti vilevile ilidhinisha ripoti hiyo jana bila kuifanyia mabadiliko.

 

Premium Article

Get Full Access for Ksh299/Week.

Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Continue Reading  →
What you get
  • Unlimited access to all premium content
  • Ad-free browsing experience
  • Mobile-optimised reading
  • Weekly newsletters & digests
Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payments Kenya's most trusted newsroom since 1902
Support Independent Journalism

Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.

Journalism can't be free because the truth demands investment. At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate, factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the pursuit of credible journalism.

Pay via
M - PESA
VISA
Airtel Money
Secure Payment Kenya's most trusted newsroom since 1902

Follow The Standard on Google News

Related Topics