Michael Joseph ndiye mwenyekiti wa bodi ya KQ

Na Mike Nyagwoka

Aliyekuwa Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya Mawasiliano ya Safaricom, Michael Joseph ametwaa rasmi uwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Ndege la Kenya Airways. Joseph ambaye ametwaa wadhifa huo baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wa bodi ya shirika hilo, Dennis Awori kujiuzulu rasmi Jumatano.
Akitangaza hatua hiyo, Waziri wa Uchukuzi, James Macharia amesema Joseph ameteuliwa kutokana na tajriba ya usimamizi aliyodhihirisha katika Kampuni ya Safaricom.
Balozi Awori amekuwa akishinikizwa kuondoka na muungano wa marubani KALPA uliomlaumu kwa kutozingatia mkataba wa kurejea kazini walipogoma mapema mwaka huu. Marubani hao vilevile wamemtaka Afisa Mkuu Mtedaji, Mbuvi Ngunze kuondoka.