Kivumbi cha uongozi chaendelea kutifuka Nairobi

Na, Suleiman Yeri

Kinyang'anyiro cha ugavana Kaunti ya Nairobi kinazidi kuchacha huku Mbunge wa Dagoreti Kusini David Waweru, Mbunge Maalum Johnson Sakaja na Seneta Mike Sonko wakitangaza kubuni muungano wa kisiasa kwa jina, Team Nairobi.
Akizungumza baada ya kuhudhuria misa ya wafu katika eneo la Dagoreti, Sakaja amesema wameafikia uamuzi ambapo mmoja wao atateuliwa kuwania ugavana na mwingine naibu gavana kwenye Kaunti ya Nairobi, huku mmoja wao akiwania useneta.
Waweru amerejelea kauli yake kwamba wakazi wa Nairobi hawawezi kukubali kupendekezewa kiongozi na kuwasuta wanaotafuta uungwaji mkono kutoka kwa baadhi ya wabunge wa jiji hili.
Aidha wamesema ushirikiano baina yao unalenga kuwaletea maendeleo wakazi wa Nairobi na kuhakikisha wanashinda kiti hicho kwenye mchujo wa vyama na wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Haya yanajiri siku chache baada ya Waziri wa Maji, Eugene Wamalwa kutangaza kushirikiana na Askofu Margaret Wanjiru kwenye kinyang'anyiro hicho.