Na ,Sophia Chinyezi
TNA yataka msajili wa vyama vya siasa kusalia ofisini
Chama cha TNA kinataka Msajili wa Vyama vya Siasa kusalia ofisini hadi uchaguzi mkuu ujao utakapokamilika. Katibu Mkuu wa chama hicho Onyango Oloo amesema kumteua mtu mwingine kuchukua nafasi ya Lucy Ndung'u kutatatiza usimamizi wa uchaguzi wa mwaka ujao.
Haya yanajiri huku shinikizo zikitolewa kwa Tume ya Huduma za Umma PSC kumteua msajili mpya na wasaidizi wengine watatu. Kauli hiyo imetolewa baada ya Rais Uhuru Kenyatta kutia saini sheria ya marekebisho ya Vyama vya Siasa, ambayo inairuhusu PSC kuwateua watakashikilia nafasi hizo.