Diamond Platinamz kuwatumbuiza mashabiki wa Radio Maisha

Na, Beatrice Maganga

Mwanamziki wa nyimbo za Bongo, Diamond Platinamz siku ya Ijumaa  anatarajiwa katika kituo hiki cha Radio Maisha kuzungumza na kuwatumbuiza mashabiki wake, siku moja kabla ya kuelekea kwa tamasha ya kukata na shoka katika Chuo cha Meru Polytenchic.
Akizungumza mapema leo baada ya kuwasili nchini, mwanamziki huyo amewaahidi mashabiki wake tamasha ya kufana.
Aidha amesema sababu ya kuandaliwa kwa tamasha hizo katika Kaunti ya Meru ni kutoa fursa kwake kukutana na mashabiki wake waliyo maeneo mbalimbali ya nchi.