Building collapses - Swahili

Idadi ya watu waliofariki kufuatia kuporomoka kwa jengo lililokuwa likijengwa huko luanda Vihiga imetimia wanne. Juhudi za kusaka miili zaidi ziliendelezwa usiku kucha, miili mitatu ikipatikana chini ya vifushi vya nyumba hiyo, watu sita kufukuliwa wakiwa hai na kukimbizwa hospitali ya Maseno, kabla ya juhudi za kuwaokoa kusitishwa usiku wa manane kufuatia mvua kubwa. Naibu waziri mkuu Musalia Mudavadi aliewasili eneo la mkasa ameahidi kwamba wizara yake itahakikisha sheria madhubuti za ujenzi zimewekwa kwenye matumizi kuhakikisha mikasa kama ile imeepukwa.