IEBC Nominees - Swahili

Jopo linalolodhibiti uteuzi wa makamishna wa tume ya uchaguzi na mipaka limechapisha orodha ya watu 262 waliotuma ombi la kuwa makamisha wa tume hiyo.isaack hassan ambaye ni mwenyekiti wa tume shikilizi ya uchaguzi ni miongoni mwa watu wanne wanaowania nafasi ya uwenyekiti wa tume hiyo.pia imebainika kwamba makamishna wanane kati ya tisa wa tume hiyo wamejitokeza kuwania nyadhfa za makamishna.orodha ya majina ya wale watakaofanyiwa uchunguzi kuhusiana na tume itakayoratibu mshahara wa wabunge katika bunge la kitaifa na bunge la senate pia yamechapishwa.uchunguzi huo unatarajiwa kuanza tarehe sita mwezi huu katika jumba la county hapa jijini.