Busia sugar land controversy - Swahili

Mashirika kadhaa ya kijamii kwa ushirikiano na muungano wa harakati za maendeleo mkoani magharibi yametoa ilani ya hadi mwishoni mwa mwezi agosti kwa kampuni ya sukari ya mumias kuwaregesha wakaazi shamba la nasawe ambalo limekuwa chini ya urasimu wa kampuni hiyo huko busia.kwa mujib wa mashirika hayo yaliyoongozwa na mwanaharakati okiya omtata okoiti  shamba hilo la ekari 841 ni mali ya umma baada ya muda wake wa urasimu kumalizika mwezi juni mwaka huu.

Related Topics

busia