Dawa Gushi zateketezwa

Bodi ya dawa nchini imeteketeza dawa za mamilioni ya pesa ilizodai ni gushi baada ya kuzinasa katika kampuni moja inayozitengeneza katika eneo la viwandani hapa nairobi. Dawa hizo za mifugo zilikuwa tayari zimeanza kusambazwa katika maeneo kadhaa humu nchini na hata katika nchi jirani kama vile somalia kabla ya bodi hiyo kupata habari kuwa kampuni hiyo hutengeneza dawa gushi na hilo lilithibitishwa na matokeo ya maabara baada ya dawa hizo kufanyiwa uchunguzi. Hata hivyo maneja wa kampuni hiyo alijitetea vikali kuwa kampuni yake haikuhusika katika kutengeneza dawa hizo ghushi.

Related Topics

Dawa Fake drugs