Police recruitment - swahili

Tume inayosimamia utekelezwaji wa katiba cic imeitaja  shughuli ya kuwasajili makurutu wa polisi iliyong'oa nanga kote nchini hii leo kama ambayo haikutilia maanani usawa wa kijinsia, kwa kutowapa wanawake nafasi sawa na wanaume. Ilikuwa ni shughuli ya kwanza kabisa ya usajili wa makurutu kutekelezwa baada ya katiba mpya, hata hivyo shughuli yenyewe ilisimamiwa na kamati maalum kinyume na tume ya huduma ya polisi kama ilivyonakiliwa kwenye katiba mpya.