Huku ongezeko la visa vya malaria
vikitarajiwa kuongezeka kutokana na mvua ya masika inayonyesha kila
uchao,serikali imeanzisha kampeini dhidi ya malaria na kutoka wiki ijayo itaanzisha
operesheni ya kunyunyuzia dawa zaidi ya nyumba milioni moja katika mikoa ambayo
huathiriwa zaidi na malaria. watoto tisini na sita hufa kila siku humu nchini
na serikali inanuia kupunguza visa hivi kwa asilimia 40% kupitia operesheni
hiyo.