×
App Icon
The Standard e-Paper
Read Offline Anywhere
★★★★ - on Play Store
Download Now

Sudi kusalia korokoroni kwa siku saba zaidi

Mbunge wa Kapsaret, Oscur Sudi atalazimika kukaa korokoroni kwa siku nyingine saba ili kuwapa polisi muda wa kufanya uchunguzi kuhusu matamshi ya uchochezi yanayomkabili.  Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Nakuru, Joseph Kalu ametoa uamuzi huo akisema Sudi atalazimika kukaa huko hadi atakapotoa uamuzi wa iwapo atamwachilia kwa dhamana ama la.

Tayari mbunge huyo alikuwa amekaa katika seli za Kituo cha Polisi cha Nakuru kwa siku mbili akisubiri uamuzi wa leo wa mahakama wa iwapo ingemwachilia kwa dhamana ama la. Baadhi ya viongozi wa Tangatanga walioandamana na Sudi wakati wa kutolewa kwa uamuzi, wamesema wanaheshimu sheria na kwamba watazingatia maagizo ya mahakama hadi kesi dhidi ya mbunge huyo itakapokamilika. Seneta wa Nakuru, Susan Kihika na Mbunge wa Bahati, Kimani Ngunjiri ni miongoni mwao.

Get Full Access for Ksh299/Week
Uncover the stories others won’t tell. Subscribe now for exclusive access
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in