The Standard Group Plc is a
multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper
print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The
Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key
influence in matters of national and international interest.
Mbunge wa Kapsaret, Oscur Sudi atalazimika kukaa korokoroni kwa siku nyingine saba ili kuwapa polisi muda wa kufanya uchunguzi kuhusu matamshi ya uchochezi yanayomkabili. Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Nakuru, Joseph Kalu ametoa uamuzi huo akisema Sudi atalazimika kukaa huko hadi atakapotoa uamuzi wa iwapo atamwachilia kwa dhamana ama la.
Tayari mbunge huyo alikuwa amekaa katika seli za Kituo cha Polisi cha Nakuru kwa siku mbili akisubiri uamuzi wa leo wa mahakama wa iwapo ingemwachilia kwa dhamana ama la. Baadhi ya viongozi wa Tangatanga walioandamana na Sudi wakati wa kutolewa kwa uamuzi, wamesema wanaheshimu sheria na kwamba watazingatia maagizo ya mahakama hadi kesi dhidi ya mbunge huyo itakapokamilika. Seneta wa Nakuru, Susan Kihika na Mbunge wa Bahati, Kimani Ngunjiri ni miongoni mwao.
Premium Article
Get Full Access for Ksh299/Week.
Uncover the stories others won't tell. Subscribe now for exclusive access.
Stand With Bold Journalism.
Stand With The Standard.
Journalism can't be free because the truth demands investment.
At The Standard, we invest time, courage and skills to bring you accurate,
factual and impactful stories. Subscribe today and stand with us in the
pursuit of credible journalism.